sponsor

sponsor

Slider

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

Comments

Text Widget

Sample Text

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.

Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exercitation test link ullamco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo consequat.

Contact Form

Name

Email *

Message *

Total Pageviews

Translate

Advertise

Comments


Definition List

Definition list
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.
Lorem ipsum dolor sit amet
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Ordered List

  1. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  2. Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  3. Vestibulum auctor dapibus neque.

Column Left

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Vivamus leo ante, consectetur sit amet vulputate vel, dapibus sit amet lectus. Etiam varius dui eget lorem elementum eget mattis sapien interdum. In hac habitasse platea dictumst.

Recent Posts

Popular Post

Most Popular

Recent Tube

Wisata

News Scroll

Favourite

Event

Culture

Gallery

Rais Erdogan amekataa kukutana na Bolton

Rais Erdogan amekataa kukutana na Bolton

Mshauri wa masuala ya usalama wa Marekani John Bolton aliyejaribu kufanya mashauriano kuhusu usalama wa washirika wa kikurdi kaskazini mashariki mwa Syria inaonekana amepuuzwa na rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.
    
Türkei Ankara John Bolton, Sicherheitsberater von US-Präsident Trump mit Ibrahim Kalin (picture-alliance/Anadolu Agency/S. Sagirkaya)
John Bolton, kushoto, na Ibrahim Kalin
Rais Erdogan amesema leo (08.01.2019) Uturuki haiwezi kukubali kauli ya hivi karibuni ya John Bolton, mshauri wa usalama wa rais wa Marekani Donald Trump, kwamba serikali ya mjini Ankara lazima ihakikishe usalama wa Wakurdi, ambao ni washirika wa Marekani. Akizungumza na wanachama wa chama cha AP bungeni, Erdogan amesema Bolton ameteleza.
"Kuhusu suala hili Bolton amefanya kosa kubwa, na anayefikiria namna hii pia amefanya kosa. Hatuwezi kubadili msimamo wetu kuhusu suala hili. Wale ambao ni sehemu ya ukanda wa ugaidi nchini Syria watapata funzo wanalostahiki. Hakuna tofauti hata moja kati ya PKK, YPG, PYD na Daesh."
Rais Erdogan aidha amesema Uturuki kwa kiwango kikubwa imekamilisha maandalizi ya kufanya harakati ya kijeshi dhidi ya kundi linalojiita dola la kiislamu IS nchini Syria. Uturuki inasisitiza hatua zake za kijeshi zinawalenga wapiganaji wa kikurdi nchini Syria, YPG, inaowachukulia kama magaidi, na wala sio raia wa kikurdi.
Bolton amekutana kwa kipindi cha takriban masaa mawili na mwenzake wa Uturuki, Ibrahim Kalin, na maafisa wengine wa ngazi ya juu lakini hakupata hakikisho lolote kuhusu usalama wa wakurdi, sharti muhimu katika mpango wa rais Trump kuwaondoa wanajeshi wa Marekani kaskazini mashariki mwa Syria.
Türkei Präsident Recep Tayyip Erdogan in Ankara (picture-alliance/Anadolu Agency/V. Furuncu)
Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki
Bolton pia amewasilisha ujumbe wa rais Trump akisisitiza Uturuki iache kuwashambulia wapiganaji wa vikosi vya kikurdi walioshirikiana na wanajeshi wa Marekani kupambana na wanamgambo wa kundi la dola la kiislamu, jambo ambalo Uturuki haiko tayari kulikubali.
Erdogan akataa kukutana na Bolton
Mshauri huyo anatarajiwa kuondoka Uturuki bila kukutana na rais Erdogan, mkutano ambao maafisa wa Marekani walisema Jumamosi iliyopita kwamba ulitarajiwa.
Msemaji wa Bolton, Garetth Maquis amesema maafisa wa Marekani wamefahamishwa kuwa Erdogan hangeweza kukutana naye kutokana na kipindi cha uchaguzi wa serikali za mitaa na hotuba aliyotakiwa kuitoa bungeni hivi leo.
Wakati haya yakiarifiwa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Marekani, Mike Pompeo, amewasili mjini Amman nchini Jordan, kituo chake cha kwanza cha ziara ya siku nane Mashariki ya Kati inayonuia kuonyesha mshikamano na eneo hilo baada ya rais Trump kutangaza kuwaondoa wanajeshi wa Marekani kutoka Syria.
Pompeo anatarajiwa kutoa hotuba kuhusu sera ya Mashariki ya Kati nchini Misri, ambako rais wa nchi hiyo, Abdel Fatah al Sisi amekuwa mshirika muhimu wa Trump. Waziri huyo wa mambo ya kigeni wa Marekani atazuru pia Manama, Bahrain, Abu Dhabi, Falme za Kiarabu, Doha, Qatar, Riyadh Saudi Arabia, Muscat Oman, Kuwait na pengine Baghdad, Iraq.
Mwandishi: Josephat Charo/afpe/ape
Mhariri: Caro Robi

Trump azungumzia hali katika mpaka wa Mexico na Marekani

Rais wa Marekani, Donald Trump amesema hali iliyopo katika mpaka wa Marekani na Mexico inazidi kuwa mbaya na imegeuka kuwa mzozo. Kauli hiyo ameitoa jana usiku katika Ikulu ya Marekani wakati akilihutubia taifa. Trump amesisitiza kuwa hatua ya kushindwa kuwadhibiti wahamiaji haramu, inawaumiza mamilioni ya wananchi wa Marekani. Amesema mzozo wa kibinaadamu na kiusalama unaongezeka katika mpaka huo uliopo kusini mwa Marekani. Rais Trump amesema kila siku maafisa wa forodha na walinzi wa mpakani wanakabiliana na maelfu ya wahamiaji haramu wanaojaribu kuingia nchini Marekani. Kiongozi huyo amerudia wito wake wa kujengwa ukuta katika mpaka huo, akisema ni muhimu kwa usalama kwenye mpaka huo. Spika wa Baraza la Wawakilishi, Nancy Pelosi amemuonya Trump aache kuishikilia serikali ya Marekani mateka kwa kutengeneza mzozo kwenye mpaka huo na amemtaka azifungue baadhi ya shughuli za serikali ambazo zimefungwa.

Maandamano dhidi ya Rais wa Sudan yaendelea

Omar al Bashir: Maandamano dhidi ya Rais wa Sudan yaendelea


Waandamanaji Khartoum 7 Januari, 2019Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Mamia ya watu wameandamana mashariki mwa mji wa Sudan wa al- Gadarif, huku maandamano ya dhidi ya Rais wa nchi hiyo Omar al Bashir yakiingia katika wiki ya tatu.
Mashuhuda wanasema kuwa majeshi ya ulinzi yametumia mabomu ya kutoa machozi kutawanya kundi la watu, ambao walikuwa wakiimbia wakisema Uhuru, Amani na Mapinduzi kwa Sauti ya Wananchi.
Maandamano hayo yaliandaliwa na Jumuiya ya Maprpfesa nchini Sudan, ambayo inamtaka Rais Bashir kujiuzulu.
Akizungumza katika kituo cha jeshi katika mji wa Atbara, kiongozi huyo amelaani kile alichokiita usaliti wa kuchoma mali kwa makusudi na kusababisha madhara.
Omar Al BashirHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRais Omar Al-Bashir
Wakati huo huo Uingereza, Marekani, Canada na Norway zimetoa taarifa ya pamoja, zikisema kwamba zimeshtushwa na taarifa za vifo na kujeruhiwa kwa watu walioshiriki maandamano hayo ya kudai haki zao.
Taarifa hiyo imedai pia kusikitishwa na utumiaji wa silaha za moto unaodaiwa kufanywa dhidi ya waandamanaji.
Katika hatua nyingine maandamano ya kuiunga mkono serikali yanaweza kufanyika leo katika mji mkuu wa nchi hiyo Khartoum.
Maandamano ya kuipinga serikali kwa mara ya kwanza yalianza katikati mwa mwezi Desemba mwaka jana kufuatia kupanda kwa gharama ya maisha.
Bei ya mkate ilipanda mara tatu katika baadhi ya maeneo na bei ya mafuta pia ikapanda.

Tetesi za Soka Ulaya Jumatano 09.01.2019: Gonzalo Higuain, Christian Eriksen, Koulibaly, Icardi, Luka Modric, Joe Hart, Ander Herrera

Tetesi za Soka Ulaya Jumatano 09.01.2019: Gonzalo Higuain, Christian Eriksen, Koulibaly, Icardi, Luka Modric, Joe Hart, Ander Herrera




Gonzalo HiguainHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionGonzalo Higuain

Chelsea wanakaribia kumsaini mshambuliaji wa AC Milan na Argentina Gonzalo Higuain, 31. (Marca)
Mwenyekiti wa klabu ya Tottenham Daniel Levy anasema kiungo wa kati wa Denmark anayeichezea klabu hiyo Christian Eriksen, 26, thamani yake ni £225m . Mchezaji huyo amekuwa akitafutwa na Real Madrid. (AS)
Mshambuliaji Mhispania aliyechezea Tottenham zamani Fernando Llorente, 33, amepewa nafasi ya kurejea Athletic Bilbao. (Mirror)
Mkuu wa Athletic Bilbao Rafael Alkorta amethibitisha kwamba anamtaka kiungo wa kati wa Manchester United na Uhispania Ander Herrera, 29, arejee katika klabu hiyo. Herrera aliihama klabu hiyo ya Uhispaniamwaka 2014. (Cadena Ser, kupitia Mail)


Christian EriksenHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionChristian Eriksen

Lakini huenda Herrera bado akasalia Old Trafford baada ya kaimu meneja wa United Ole Gunnar Solskjaer kudaiwa kumshawishi asalie katika klabu hiyo. (Sun)
Manchester United wamekubali kwamba itawalazimu kusubiri hadi mwisho wa simu ndipo waweze kumpata beki wa kati wa Napoli na Senegal Kalidou Koulibaly, 27. (ESPN)
Meneja wa zamani wa Arsenal Arsene Wenger ameombwa kuwa mkufunzi wa timu ya taifa ya Qatar. (France Football)
Inter Milan wako tayari kumuuza mshambuliaji wa Croatia Ivan Perisic, 29, kwa Manchester United ndipo waweze kupata pesa za kumnunua kiungo wa kati wa Real Madrid ambaye pia anatokea Croatia Luka Modric, 33. (Tuttosport, kupitia Calciomercato)
Mshambuliaji wa Inter Milan na Argentina Mauro Icardi, 25, ni miongoni mwa wachezajia ambao mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich anataka kuwanunua mwezi huu. (Mirror)
Bayern Munich wameongeza kitita ambacho wako tayari kutoa kumchukua mshambuliaji wa Chelsea Callum Hudson-Odoi hadi £35m. Mchezaji huyo wa miaka 18 amekariri hamu yake ya kutaka kuihama klabu hiyo ya Stamford Bridge mwezi huu. (Guardian)


Callum Hudson-OdoiHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionCallum Hudson-Odoi alijiunga na Chelsea mwaka 2007

Chelsea wanamtaka mshambuliaji wa AC Milan kutoka Ureno Andre Silva - ambaye yupo Sevilla kwa mkopo - lakini uhamisho huo utategemea the Blues kukubali mshambuliaji wao wa Uhispania Alvaro Morata ahamie klabu hiyo ya Sevilla. (Sun)
Everton wanamnyatia kiungo wa kati wa Porto na Algeria Yacine Brahimi na walimtuma skauti kumfuatilia Jumatatu wakati wa mechia ambayo walishinda 3-1 dhidi ya Nacional. Kiungo huyo wa miaka 28 alifunga mabao mawili mechi hiyo. (Mirror)
Kipa wa Burnley Joe Hart, 31, anatafutwa na klabu ya Preston ambao wanamtaka kwa mkopo. (Sun)
Crystal Palace wanamtaka mshambuliaji wa Chelsea Tammy Abraham ajiunge nao kwa mkopo baada ya mchezaji huyo wa miaka 21 ambaye kwa sasa yupo Aston Villa kwa mkopo kukataa fursa ya kujiunga na Wolves. (Mirror)


Tammy Abraham in action for Aston VillaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionTammy Abraham

Southampton wanataka sana kumsaini mshambuliaji wa Everton Ademola Lookman, 21. (Star - via HITC)
Fulham waliwatembeza beki wa England Gary Cahill, 33, winga wa Nigeria Victor Moses na kiungo wa kati wa England Danny Drinkwater, wote wawili wakiwa na miaka 28, katika uwanja wao wa mazoezi katika juhudi za kutaka kuwashawishi kujiunga nao kutoka Chelsea. (Love Sport Radio)


Gary CahillHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionGary Cahill

Beki wa Liverpool Rafael Camacho, 18, anatarajiwa kuondoka Anfield - siku chache tu baada yake kuchezeshwa mara ya kwanza katika timu kuu. Sporting Lisbon wanadaiwa kuwa karibu kuafikiana na Liverpool kuhusu beki huyo wa kulia. (Talksport)
Newcastle wanatafakari uwezekano wao wa kujiondoa kutoka kwenye mchakato wa kumnunua kiungo wa Atlanta United Miguel Almiron. Klabu hiyo ya St James' Park. inasema ujira anaodai mchezaji huyo wa miaka 24 kutoka Paraguay ni wa juu mno. (Talksport)
Kiungo wa kati wa Watford Abdoulaye Doucoure amekiri kwamba anataka sana kuhamia kwa miamba wa Ufafaransa Paris St-Germain, ambao wameonyesha nia ya kumtaka mchezaji huyo wa miaka 26. (Mirror)
Kiungo wa kati wa Tottenham na Ubelgiji Mousa Dembele, 31, anakaribia kuhamia klabu ya Ligi Kuu ya China ya Beijing Guoan, uhamisho ambao utakuwa wa £11m. (Talksport)
Kiungo wa kati wa Barcelona Denis Suarez, 25, anataka kuhamia Arsenal mwezi hu wa Januari, ingawa klabu yake awali haikutaka kumwachilia. (Mirror)


Denis Suarez scores for BarcelonaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionDenis Suarez (kushoto)

Spurs wanatarajiwa kufanya mazungumzo na mshambuliaji wao kutoka Uholanzi Vincent Janssen ambaye amekuwa hachezeshwi sana, na wanataka kumwacha mshambuliaji huyo wa miaka 24 aondoke Januari. (Mail)
Beki wa kati anayechezea Burnley Jimmy Dunne, 21, anatafutwa na Sunderland kwa mkopo. (Burnley Express)
Reading wamekataa ofa ya £450,000 kutoka Wigan ambao wamekuwa wakimtaka beki Tyler Blackett, 24. (Mail)
Preston na West Brom wote wanamtaka kiungo wa kati wa Mansfield CJ Hamilton, 23. (Mansfield Chad)
Newcastle wamekataa ofa kutoka kwa West Brom ambao wamekuwa wakimtaka kiungo wa kati Isaac Hayden, 23. (Express & Star)
Aston Villa pia wanadaiwa kujitosa katika mbio za kumtaka Hayden. (Mirror)
Arsenal wanatafakari uwezekano wao wa kumteua kiungo wa kati wa zamani Edu kuwa mkurugeniz wao mpya wa uchezaji. Mbrazil huyo alistaafu soka mwaka 2010. (Standard)


Isaac HaydenHaki miliki ya pichaREX FEATURES
Image captionIsaac Hayden

Barcelona wako radhi kumuuza winga wao kutoka Brazil Malcom, 21, ingawa walimnunua majira ya joto yaliyopita. (Mundo Deportivo)
Tottenham wanamfuatilia kwa karibu beki kamili wa Wolves Matt Doherty ingawa mchezaji huyo wa miaka 26 huenda akaongezewa ujira wake maradufu katika klabu hiyo ya Molineux wiki chache zijazo. (Irish Independent)
West Ham wanatarajiwa kuimarisha ofa yao ya kutaka kumnunua kiungo wa kati wa zamani wa Cardiff Gary Medel. Mchezaji huyo wa miaka 31 kutoka Chile anatarajiwa kuihama Besiktas iwapo kutatokea klabu iliyo tayari kutoa pesa zinazofikia makadirio ya thamani yake. (Takvim - kupitia Sport Witness)

Bora kutoka Jumanne



Philippe CoutinhoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionPhilippe Coutinho alihamia Barcelona kutoka Liverpool

Manchester United wameanzisha mazungumzo na Barcelona wakitaka kumsajili mshambuliaji Mbrazil Philippe Coutinho, 26, lakini ndipo waweze kumnasa itabidi wachomoe zaidi ya £100m. (Caught Offside)
Sevilla wamefanya mazungumzo na Chelsea kuhusu kumchukua mshambuliaji wa Uhispania Alvaro Morata, 26, kwa mkopo hadi mwisho wa msimu huu. (Goal.com)
AC Milan wanamtafuta mshambuliaji wa Genoa na Poland Krzysztof Piatek, 23, wakitaka kumtumia kujaza pengo litakaloachwa na mshambuliaji wa Argentina Gonzalo Higuan, 31. (La Gazzetta dello Sport)
Uhamisho wa Cesc Fabregas kwenda Monaco unakwamishwa na hali kwamba klabu hiyo ya Ligue 1 bado haijaafikiana na klabu ya Chelsea kuhusu ada ya uhamisho wa kiungo huyo wa kati wa Uhispania mwenye miaka 31. (London Evening Standard)


Cesc FabregasHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionCesc Fabregas

Meneja wa Chelsea Maurizio Sarri amemshauri Fabregas kuihama klabu hiyo ya Stamford Bridge kwa maslahi ya uchezaji wake. (Talksport)
Juventus wanasema wanaweza wakashawishika kumuuza Paulo Dybala, 25, ambaye anatafutwa na Manchester City mwisho wa msimu, lakini mradi tu ada ya uhamisho wa raia huyo wa Argentina iwe zaidi ya £90m. (Tuttosport kupitia Express)


Paulo DybalaHaki miliki ya pichaEPA
Image captionPaulo Dybala

Atletico Madrid wamekataa ofa kutoka kwa Manchester United waliokuwa wanamtaka beki wa Uruguay Diego Godin, 32. (Tutto Mercato Web)
Beki wa Ajax anayechezea timu ya taifa ya Uholanzi Matthijs de Ligt, 19, amehimizwa kukataa kuhamia Juventus na badala yake ajiunge na Manchester United. (Manchester Evening News)
Real Madrid wameanza harakati za kutaka kumsajili mshambuliaji wa Denmark Christian Eriksen, 26, kutoka Tottenham na wanajiandaa kutoa takriban £100m kumnasa. (Independent)